Posts

Showing posts from December, 2017

TETESI ZA SOKA LA ULAYA JUMAPILI HII 17/12/2017

Image
         Jonny Evans. Manchester United wanataka kumleta mlinzi Jonny Evans Old Trafford, miaka miwili unusu baada ya kumuuza mchezaji huyo wa miaka 29 kwenda West Brom, lakini Manchester City na Arsenal wanammezea mate. Juventus wanaonekana kuwa na nia ya kumuuza mlinzi Alex Sandro lakini Chelsea walioshindwa kumsaini mbrazil huyo msimu huu, wanakabiliwa na ushindani kutoka Manchester City, Manchester United na Paris St-Germain.                                                        Klopp. Daniel Sturridge ameambiwa anaweza kuondoka Liverpool kwa mkopo mwezi ujao na meneja Jurgen Klopp wakati mchezaji huyo wa miaka 28 raia wa England anataka kujitafutia nafasi katika kombe la dunia . Meneja wa Liverpool anasema kuwa alishinikizwa na maajenti wake kumsaini Mohamed Salah msimu huu baada ya hofu kuwa wing'a huyo wa Misri wa umri wa miaka 25 alikuwa mdogo sana kuweza kufanikiwa katika Premier League. Mohamed Salah. Manchester United wanatathmini ikiwa watatoa of

WAJUMBE WA ANC WAKUTANA KUMCHAGUA KIONGOZI MPYA

Image
Chama tawala cha ANC nchini Afrika kusini kinafanya mkutano mkuu kumteua kiongozi mpya wa chama hicho. Rais Jacob Zuma amekiongoza chama hicho kwa muongo mmoja sasa. Chama hicho tawala kimekuwa kikipoteza umaarufu kutokana na kashfa za rushwa na tofuati za ndani ya chama chenyewe. Lakini bado kina umaarufu katika ulingo wa kisiasa baad ya kuwepo madrakani kwa miaka 23. Kikao hicho kinakutanaisha wajumbe takriban elfu tano mjini Johannesburg. Rais Jacob Zuma wa Afrika kusini anatarajiwa kuhutubia wajumbe wanaohudhuria mkutano huo mkuu.                                   Wagombea wakuu. Wajumbe wanatarajiwa pia kuwachagua viongozi sita wa ngazi ya juu kuanzia rais wa chama hadi naibu katibu mkuu wa chama. Kivumbi hasa kipo katika Kinyanganyiro cha kumrithi rais Zuma, kama kiongozi wa chama- ni kati ya mkewe wa zamani Bi Nkosazana Dlamini-Zuma -- ambae pia aliwahi kuwa waziri na vilevile alikuwa mwenyekiti wa umoja wa Afrika. Lakini anakabiliwa na upinzani mkali kutok

MNADA WA TATU WA KIMATAIFA WA MADINI YA TANZANITE KUFANYIKA MERERANI

Image